Tuesday, March 8, 2011

Kwanini Wanawake Warembo Hupenda Kuolewa na Wanaume Wenye Sura Mbaya????


WANAWAKE wengi waliowazuri wa sura huwa wanapenda kuolewa na wanaume wabaya wa sura. Hii inatokana na ukweli kwamba wanawake wenye sura nzuri hupenda kuolewa na wanaume wenye sura mbaya ili kulinda uzuri wao kwani wanaamini kuwa iwapo ataolewa na mwanaume mwenye sura nzuri, uzuri wake hautaonekana kwa watu kwani mwanaume pia ataonekana mzuri jambo ambalo litamupunguzia mwanamke kuonekana mzuri katika jamii. Hii ndio maana wanawake wengi wenye sura nzuri wanapenda kuolewa na wanaume wenye sura mbaya. Dr. Linda Mtaalamu wa masuala ya mapenzi na uhusiano anasema " Wanawake wengi wenye sura nzuri wanatabia ya kutaka waonekane kuwa ni warembo, jambo ambalo linawapelekea kuolewa na wanaume wenye sura mbaya ili waendelee kushine katika jamii".

Pia wanaume wenye sura mbaya wanapenda kuoa wanawake wenye sura nzuri ili kulinda hishima yao kwa kupitia  wake zao. Kwahili ndugu msomaji naomba ujaribu kufanya uchunguzi wa kina kwa kuangalia wanaume wenye sura mbaya, utagundua kuwa wengi wao wanapenda kuoa wanawake wazuri na wengi wao tayari wameshaoa wanawake warembo. Je, kwa upande wa wanawake weusi; je, wanapenda wanaume wa aina gani? Na kwa upande wa wanaume weusi pia wanapenda wanawake wa aina gani? Pia na wewe kama unajitabua kuwa uko hivi au vile je, unapenda sweetheart wako aweje. Sasa tujadili.........................!!!!!

Tabia za Mwanamke


LEO nitaongelea kuhusiana na tabia za mwanamke. Tabia za mwanamke hasa katika suala zima la mapenzi ni kwamba mwanamke ni kiumbe kilichoumbwa kwa namna tofauti kabisa, kwani anauwezo mkubwa sana wa kumtambua mwanaume muongo au laghai wa mapenzi pia mwanamke ni binadamu aliyemvumilivu sana hasa akijua kuwa mume wake ni mwaminifu kwake kwa hili nakuoma Ndg. msomaji ebu jaribu kufanya  uchunguzi juu ya jambo hili.

Pia mwanamke katika mapenzi au ndoa huwa ni binadamu aneyependa sana kufarijiwa na kupewa pole kwa kila kitu ambacho kinaonekana kimemuumiza. Mwanasaikolojia mtaalamu wa masula ya mapenzi Dr. Linda wa chuo kikuu cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema "Female needs to be satisfied by Male in each and every things" Kwa mujibu wa Linda mwanamke ni kiumbe kinachohitaji kurizishwa kwa kila kitu, kwa hiyo ndugu zangu inawapasa kuhakikisha unamurizisha mkeo ili  kujenga penzi la kudumu.