Tuesday, March 8, 2011

Kwanini Wanawake Warembo Hupenda Kuolewa na Wanaume Wenye Sura Mbaya????


WANAWAKE wengi waliowazuri wa sura huwa wanapenda kuolewa na wanaume wabaya wa sura. Hii inatokana na ukweli kwamba wanawake wenye sura nzuri hupenda kuolewa na wanaume wenye sura mbaya ili kulinda uzuri wao kwani wanaamini kuwa iwapo ataolewa na mwanaume mwenye sura nzuri, uzuri wake hautaonekana kwa watu kwani mwanaume pia ataonekana mzuri jambo ambalo litamupunguzia mwanamke kuonekana mzuri katika jamii. Hii ndio maana wanawake wengi wenye sura nzuri wanapenda kuolewa na wanaume wenye sura mbaya. Dr. Linda Mtaalamu wa masuala ya mapenzi na uhusiano anasema " Wanawake wengi wenye sura nzuri wanatabia ya kutaka waonekane kuwa ni warembo, jambo ambalo linawapelekea kuolewa na wanaume wenye sura mbaya ili waendelee kushine katika jamii".

Pia wanaume wenye sura mbaya wanapenda kuoa wanawake wenye sura nzuri ili kulinda hishima yao kwa kupitia  wake zao. Kwahili ndugu msomaji naomba ujaribu kufanya uchunguzi wa kina kwa kuangalia wanaume wenye sura mbaya, utagundua kuwa wengi wao wanapenda kuoa wanawake wazuri na wengi wao tayari wameshaoa wanawake warembo. Je, kwa upande wa wanawake weusi; je, wanapenda wanaume wa aina gani? Na kwa upande wa wanaume weusi pia wanapenda wanawake wa aina gani? Pia na wewe kama unajitabua kuwa uko hivi au vile je, unapenda sweetheart wako aweje. Sasa tujadili.........................!!!!!

10 comments:

Masangu Matondo Nzuzullima said...

Wanaume nao kwa upande wao....

http://matondo.blogspot.com/2010/10/utafiti-wanaume-huvutiwa-zaidi-na-sura.html

Simon Kitururu said...

Hii kitu sio rahisi kihivyo kwa kuwa naamini swala la uzuri na ubaya sio rahisi kihivyo kitu kifanyacho nishashuhudia mwenyewe anikiringiwa na mtu ambaye matamanio ni ziro ingawa anajiamini namtamani !


Naamini hii kitu ni ngumu kuirahisisha kihivyo!
Ni mtazamo tu wangu!

Fita Lutonja said...

Ok asanteni sana kwa maoni yenu mazuri

Anonymous said...

Kwa ajili asimuonee wivu mume wake kwa wanawake wengine.

Mija Shija Sayi said...

Aaaaah! Kaka Lutonja hapa sikubaliani na wewe kabisaa labda utupe mifano halisi..

Asante kwa mada motomoto..

Rachel Siwa said...

Uzuri wa mtu anaujua mtu,kwani mzuri kwako kwa mwingine si mzuri!inategemea wewe umependea mguu wake na Kitururu kapendea nywele!.

sikudhani khamis said...

me ninachojua uzur na ubaya wa mtu upo machon kwa mtu, kwahyo wewe unaweza kumuona huyu mtu kama mbaya lakin mwenzio anaona kawaida au mzuri sana

Unknown said...

Nadhani kwa Upande wa Mwanamke nzuri anapo olewa na Mwanamume ambaye sio nzuri, mara nyingi hufuata HELA na si tu kutaka uzuri wake uendelee kuonekana ILA kwa Mwanamume huaga tofauti kidogo mara nyingi Mwanamume hupenda kuwa na mwanamke nzuri kwa ajili tu ya kujionyesha na kujipatia sifa kwa Rafiki zake na hata jamii kwa ujumla. na mara nyengine ni KUAMINI kuwa mwanamke nzuri atakuzalia watoto wazuri watakao kupa hadhi kwa kupata waume wenye hea.

HoliestLife Ministry said...

Kazi ya Mungu ni njema ktk uumbaji. Hakuna makosa wala mapungufu ktk kazi yake ya kumuumba mwanadamu, hata yule aliyezaliwa kilema ni ni ili kazi/uweza wake upate kudhihirika. Kwa ww uliyeumbwa,(mwanadamu) Mungu hakupi vyote na pia hakunyimi vyote, hivyo basi ridhika na jikubali jinsi ulivyo na mshukuru MUNGU.

Hamis Rashid said...

Habari hii binafsi naona kama wanawake wazuri wapo special kwa kupiga pesa kwani uzuri wa mwanaume kwao sio kigezo katika maisha yao.