Thursday, May 21, 2009

Penzi la Wahindi

KARIBU tena ndugu zangu leo napenda kujua zaidi kuhusiana na mwananke wa kihidi na wakiafrika nani mzuri zaidi na nani anahusudu mapenzi kuliko. Kwani kumekuwepo na mkanganyiko wengine wanasema wahindi wanabaridi sana wengine wanasema waafirika wanajoto sana je, ni kweli? Wengine wafrika ni wazuri wengine wahindi ni wazuri. Sasa tujadili kupitia maoni yenu.

Mwingine anapenda wachaga wengine wasukuma


BINADAMU wote ni sawa lakini tunatofautiana kimawazo, fikra, kiutendaji, kipawa nk. Haya nilikuja kuyadhitisha katika kufuatilia fikra za Mwanafalsafa aliyekuwa maarufu sana kwa uchambuzi wa fikra na mawazo ambaye alikuwa anaitwa Plato.
Katika kazi yake ya "Republic" Plato alisema kuwa kila binadamu ameubwa tofauti kutokana na wengine kuwa na akili nyingi ambaye yeye aliwaita "golden boy" ambao yeye hawa aliwaelezea kuwa ni wale wanaweza kuwa viongozi wa nchi yaani (Philosphers, Gvern Planners and Rulers)

Wengine wanaakili ya kawaida "Silver boy" kwa mujibu wa Plato hawa ni wale wanaotakiwa kuwa walinzi wa nchi yaani askali jeshi na polisi pia alisema kundi la mwisho wa wale ambao wanaakili finyu "Iron Boy "hawa Plato alisema kuwa kwa kuwa wanauwezo mdogo wa kupambanua mambo kazi yao ni kulima na kuwa wazalishaji wa bidhaa za nchi.

Hii ilikuja pale nilipojaribu kufanya uchunguzi wangu na kugundua kuwa kumbe hata katika suala la upendo binadamu tuko tofauti wengine wanapenda wanene wengine wembamba na wengine weupe wengine weusi.

Katika makabira wengine wanapenda kabira fulani, kama mimi ninapenda wachaga na wengine hawapendi wachaga wengine wasomi wengine hawapendi wasiomi kwahiyo kutokana na hili binadamu tuko tofauti.

Je, katika mtazamo wako wewe unaona je? tujadili.

Wednesday, May 20, 2009

Mwanafalsafa Socrates alihusudu ndoa


SIKU moja nilikuwa naelekea kwenye press conference moja tukiwa na rafiki yangu ambaye ni mwanahabari mwenzangu tulipofika maeneo ya Magomeni akaniambia kuwa anataka kuoa nami nikatafakari kwa kina maelezo kisha nikamjibu kuwa ni jambo jema kuoa kwani kuwa na mke ni mojawapo ya maisha tuliopangiwa na Mungu.


Mara nikakumbuka usemi wa Mwanafalsafa wa Kigiriki aitwaye Socrates naye alidhamini sana ndoa kwani aliwahi kusisitiza kuwa kama ukiona maisha ni magumu ni vizuri kuoa mwanamke Mzuri. "If you see life is hard you have to find a good wife to refresh your mind" alisema Socrates.


Jambo la kuwa na Mwanamke ni mhimu sana kwani watu wengi hasa katika nchi zinazoendelea huwa wanapata msongo wa mawazo kutokana na maisha kuwa magumu lakini Mwanasayansi Samuel Spire anasema kuwa kuwa na Mwanamke ni mojwapo ya kupunguza msongo huo wa mawazo.


Anasema kuwa mwanamke anasaidia kuondoa msogo wa mawazo kwa mwanaume vilevile mwanaume anasaidia kuondoa msongo wa mawazo kwa mwanamke. Hii inatokana na homoni zinazotolewa pindi mwanaume au mwanake anapokuwa na mpenzi wake.


Je , wewe ndungu yangu ulishawahi kukutana na msongo wa mawazo baadaye ulipomuona mpenzi wako ukajisikia uko fresh? sasa tujadili katika kibaradha chetu.

Sunday, May 17, 2009

Falsafa na Penzi


NIMERUDI tena ndugu zangu nilikuwa masomoni kwa muda kidogo ila sasa hivi niko kazini kwangu ninachati na mhariri wangu wa habari ambaye ndiye Mwalimu wangu Mkuu katika kuhakikisha jamii inaelimika kupitia vyombo mbalimbali vya habari.
Huko masomoni nimejifunza mambo mengi sana nimejifunza kuwa kumbe watanzania waliowengi hawajui kingereza!!!! Nilishaangaa sana Mhadhiri wangu wa lugha aliponiambia hata Kenya hawajui kingereza!!
Kwa sababu fani yangu ni Kudadisi nilimhoji kwa nini anasema hivyo ? Jibu alilonipa Ahhh!!! eti katika vitabu alivyosoma hakuna sehemu ambayo amekuta kumeandikwa rafudhi ya kingereza ya Afrika Mashariki!!(East African Accent) hayo yote nimejifunza kwa sababu nilikuwa nafuatilia kwa ukaribu sana mongozi wa lugha hii ya kingereza.
Ama kweli elmu haina Mwisho kwani nilijifunza mengi sana? Ikiwa pamoja na Mhadhiri wangu wa Falsafa alinifundisha kuwa elimu haina Mwisho huku akisema elimu inaanzia mtu anapozaliwa na pale anapokufa!!. Kwasababu napenda Falsafa niliamua kuziunganisha falsafa za Mhadhiri wangu na kuzifanyia kazi.
Jambo nililogundua ni kwamba hata penzi halina mwisho pendo linadumu siku zote ila kunakumchukia mtu fulani, lakini pia ukimchukia huyu utampenda huyu ndiyo maisha ya binadamu. Je kama tusingekuwa na upendo tungeishije katika dunia hii? Sasa tujadiliane ndugu zangu.