Wednesday, March 28, 2012

JAMANI NIMERUDI TENA NILIKUWA MASOMONI

IMERUDI tena kwenye kibaraza chetu, karibuni sana nilikuwa nigeria nasoma masters ya Journalism Curriculum Development and Designing nimemaliza nimerudi TZ  coz naipenda nchi yangu japo mafisadi wananikatisha tamaa mpaka nilifikia uamuzi wa kutaka nisirudi TZ lakin rafiki yangu mpendwa Cretus  akanishauri nirudi nimefurahi kukutana na watanzania wenzangu. Hapo juu ni dada ambaye alinisaidia kuchapa RESEARCH REPORT yangu, ni dada mkarim sana hakika sitamsahau ktk maisha yangu, bila yeye yawezekana nisingemaliza masomo yangu.

Jamani nimekumbuka kitu kimoja niliambiwa na rafiki yangu ambaye tulikuwa tunasoma naye huko nje aliniambia "Tanzania ni nchi nzuri sana lakini kuna ufisadi mkuu katika sekta ya elimu hasa wanapoajiriwa walimu wapya kwani huwa hawalipwi mishahara yao miezi miwili kitu ambacho kinawafanya waishi maisha ya kuomba omba kwa wanafunzi na walimu wengine" maneno haya yalitia uchungu sana na nchi yangu. Ni hayo tu ila nawaomba tujadiri "JE NCHI YETU INATOA HAKI KWA WALIMU???????? Kazi kwenuuuuuuuuuuu.

Tuesday, April 26, 2011

WANABLOGU NAWATAKIA PASAKA NJEMA


WAPENDWA katika bwana nawatakia pasaka njema. Mimi imenikumbusha mwaka 2005 nilipoamua kuokoka na kumurudia Mungu wangu kwa nguvu zote. Ndugu zangu nakumbuka ilikuwa mwezi wa tatu mwaka wa 2005 nikiwa pale Morogoro nilipata ubatizo na kuanza kujiandaa na pasaka ila ninachokikumbuka zaidi wakati nikibatizswa na Mch Peter Denis ni pale aliponishika kichwani na kuanza kuniombea nikiwa katikati ya maji ghafra nilipatwa na nguvu furani nikajikuta nalia kwa nguvu watu wote walishutuka ila mchungaji alinifariji na kunitaka nimshukuru Mungu.

Mch Peter Denis baada ya kunifariji alinishika kichwani na kunizamisha majini nilipotoka majini nikajisikia nimezaliwa upya machozi ambayo nilikuwa nalia yakakauka na muchugaji akaniambia kwa maneno ya upendo "Asante Mwanangu Hakika Umebarikiwa" Kwakweli namkumbuka sana mchungaji wangu na Mungu amubariki sana katika kazi yake ya utumishi. Japo kwa sasa niko Da,r ila Mchungaji Peter Denis sitamsahau kwani alifungua ukurasa mpya wa maisha yangu.

Kwahiyo ndugu zangu yatupasa kumshukuru Mungu kwa kila jambo hasa katika siku hizi za sikuku za Yesu Kristo. Mungu awabariki sana wanablogu, na pia awape nguvu kwa kazi zenu, maoni yenu juu yangu yatabarikiwa pia. Ameni.

Tuesday, March 15, 2011

Si Kila Mshauri wa Mapenzi Anajua Kupenda........


SIKU moja nilikuwa katika shughuri zangu za kutoa ushauri katika suala zima la mapenzi na uhusiano katika ofisi zetu zilizoko Kiwani Bombom kijiwe Samli jijini Dar es Salaam, nilisikitika  kumuona mama mmoja akifika katika ofisi zetu huku akitokwa na machozi, yaani nilisikitika sana, sana na tena sana kwani nilipatwa na roro ya huruma.

Baada ya kuingia mama huyo alinieleza kuwa anataka ushauri juu ya mume wake kwani huyo mume wake huwa anamunyanyasa sana na kilichomfanya aje kwangu huku akitokwa na machozi ni kwa sababu mume wake alimutukana na kumwambia aondoke aende kwao. Mume wake huyo alimutaka achukue gari mbili nyumba moja, na kiwanja kilichoko Kigamboni lakini mwanamke huyo hakutaka kuondoka kwa mume wake kwani  bado anampenda sana na anamuhitaji sana na ndio maana anataka nimupe ushauri.

Nilimpa dozi kubwa ya ushauri jinsi ya kumrekebisha mwanaume mkorofi na kuwa baba mzuri mwenye upendo na familia yake. Nilimshauri mambo mengi juu ya kudumisha ndoa yake na nikamuhakikishia kuwa iwapo atafuata ushauri wangu hakika hatajutia kuja kwangu. Baada ya kumshauri sana mama huyo nilimuona kajawa na roho ya furaha sana, huzuni na majonzi aliyokuja nayo yalitoweka kama upepo na kuniona mimi kama ni mtu niliyebarikiwa na Mungu kwa kujua kushauri watu.

Mama wa watu alijikuta akinitamukia "Hakika wewe ni baba uliyejaa upendo kwa kila mtu na ninaamini mke wako anaishi kwa amani na raha tele hata kama huna pesa nyingi kama mume wangu kwani maneno yako ni matamu sana yanajenga na yanaleta amani ndani ya ndoa" aliniambia mama huyo na kuongeza  "Ukimwambia mwanamke yeyote aliyekamilika hakika yanamfariji sana, ndio maana ninakuambia kwamba wapo wanaume kama nyinyi wenye kujua upendo na ndoa ni nini? wewe ni baba pekee katika ulimwengu huu" alisisitiza mama huyo.


Lakini aliponiambia hayo nilisimama na kuvua koti langu na kuliweka katika hangs na pia nikakaa katika kiti changu, nikamtazama kwa macho ya huruma na kumtamkia kwamba mimi siyo najua kila kitu mimi ni binadamu kama wanaume wengine na ninamapungufu mengi tu, siyo tu katika maisha pia na hata katika masuala ya mapenzi na mahusiano. Kwahiyo sio kila mwanasaikolojia wa mapenzi anajua kupenda. Sasa tujadili juu ya jambo hili, Yasinta dada  yangu, Marcus kijana mpotevu, Koero mtaalam, Simon mchapakazi NK.

Tuesday, March 8, 2011

Kwanini Wanawake Warembo Hupenda Kuolewa na Wanaume Wenye Sura Mbaya????


WANAWAKE wengi waliowazuri wa sura huwa wanapenda kuolewa na wanaume wabaya wa sura. Hii inatokana na ukweli kwamba wanawake wenye sura nzuri hupenda kuolewa na wanaume wenye sura mbaya ili kulinda uzuri wao kwani wanaamini kuwa iwapo ataolewa na mwanaume mwenye sura nzuri, uzuri wake hautaonekana kwa watu kwani mwanaume pia ataonekana mzuri jambo ambalo litamupunguzia mwanamke kuonekana mzuri katika jamii. Hii ndio maana wanawake wengi wenye sura nzuri wanapenda kuolewa na wanaume wenye sura mbaya. Dr. Linda Mtaalamu wa masuala ya mapenzi na uhusiano anasema " Wanawake wengi wenye sura nzuri wanatabia ya kutaka waonekane kuwa ni warembo, jambo ambalo linawapelekea kuolewa na wanaume wenye sura mbaya ili waendelee kushine katika jamii".

Pia wanaume wenye sura mbaya wanapenda kuoa wanawake wenye sura nzuri ili kulinda hishima yao kwa kupitia  wake zao. Kwahili ndugu msomaji naomba ujaribu kufanya uchunguzi wa kina kwa kuangalia wanaume wenye sura mbaya, utagundua kuwa wengi wao wanapenda kuoa wanawake wazuri na wengi wao tayari wameshaoa wanawake warembo. Je, kwa upande wa wanawake weusi; je, wanapenda wanaume wa aina gani? Na kwa upande wa wanaume weusi pia wanapenda wanawake wa aina gani? Pia na wewe kama unajitabua kuwa uko hivi au vile je, unapenda sweetheart wako aweje. Sasa tujadili.........................!!!!!

Tabia za Mwanamke


LEO nitaongelea kuhusiana na tabia za mwanamke. Tabia za mwanamke hasa katika suala zima la mapenzi ni kwamba mwanamke ni kiumbe kilichoumbwa kwa namna tofauti kabisa, kwani anauwezo mkubwa sana wa kumtambua mwanaume muongo au laghai wa mapenzi pia mwanamke ni binadamu aliyemvumilivu sana hasa akijua kuwa mume wake ni mwaminifu kwake kwa hili nakuoma Ndg. msomaji ebu jaribu kufanya  uchunguzi juu ya jambo hili.

Pia mwanamke katika mapenzi au ndoa huwa ni binadamu aneyependa sana kufarijiwa na kupewa pole kwa kila kitu ambacho kinaonekana kimemuumiza. Mwanasaikolojia mtaalamu wa masula ya mapenzi Dr. Linda wa chuo kikuu cha Havard nchini Marekani aliwahi kusema "Female needs to be satisfied by Male in each and every things" Kwa mujibu wa Linda mwanamke ni kiumbe kinachohitaji kurizishwa kwa kila kitu, kwa hiyo ndugu zangu inawapasa kuhakikisha unamurizisha mkeo ili  kujenga penzi la kudumu.

Monday, March 7, 2011

Wanablugu Nimerudi Tena

NIMERUDI tena baada ya kutingwa na kazi nyingi sana! Ila kwa sasa nimerudi kwenye chakula chetu cha kila siku nilikimis sana nilikuwa nakosa nguvu kwa sababu ya kukosa chakula chetu kwa wale ambao wanataka kujua nilikuwa wapi? Nilikuwa nimebanwa na jamaa mmoja anayeitwa muda hakika nilikuwa mutumwa wa muda kila kitu huyu muda alikuwa ananiamulisha! lo! Nimekoma na huyu muda!Hakiaka angekuwa anaonekana ningemkomoa kwelikweli! Ila nawapenda wote wanablogu wenzangu mmmwaaaaaa!!

Sunday, December 12, 2010

Uchungu wa Penzi

Watu wengi hutoa machozi pale wanapoachwa na wapenzi wao, Mpenzi msomaji wa blogu yako uipendayo ya saikolojia leo nitakueleza kuhusiana na chozi la penzi: Unajua wataalamu wa mambo ya mapenzi wanasema kuwa Mwanamke ni mwepesi sana kutoa machozi pindi anapoachwa na mpenzi wake hii inatokana na mwanamke kuubwa na moyo wa kuwa na penzi la rohoni.

Wataalamu wa mambo ya mahaba wanasema kuwa wanawake wameumbwa kwa penzi la rohoni yaani la ndani tofauti na wanaume, hii ndiyo inasababisha mwanake akiachwa na mpenzi wake hujisikia vibaya na kujiona kama hafai kabisa kwa mwanaume yoyote kitendo ambacho kinamfanya anatoa machozi kwa wingi sana.

Mwanaume kaumbwa kwa penzi la fikra kama wanavyotufahamisha wataalamu wa mapenzi hii ndiyo maana wanaume wengi ni vigumu sana kulia pale wanapoachwa na wapenzi wao japo wapo wanaolia lakini sio wengi japokuwa huwa wanaumia sana rohoni lakini kutokana na elementi walizoumbwa nazo inakuwa vigumu kutoa machozi. "Nakusihi uendelee kuburudika zaidi na blogu yako usisahau kutoa maoni"

Sunday, November 21, 2010

Harufu ya Wizi Yanukia UDOM

Makamu mkuu wa  chuo Prof. Idrisa Kikula
LEO wapenzi wa blogu hii nitaongelea kidogo kuhusu wanafunzi wa chuo Kikuu cha Dodoma  (Udom), katika hali ya kushangaza na kusikitisha na pengine kupelekea kuathiri kisaikolojia katika hali ya kufikiri na kujiwekea malengo kwa wanafunzi hao.

Katika pitapita zangu kama mwandishi wa habari nilikutana na wanafunzi hao na waliponiona tu, wakanipokea kwa shangwe sana huku sura zao zikionyesha kupata furaha ya kuniona, nami kwa hali kama hiyo nilijikuta nawauliza kulikoni kisaikolojia wanaonekana kufadhaika sana?. Lakini kwa sura za huzuni wakanijibu.

"Kaka tunasikitishwa sana na harufu ya wizi inayotukabili katika chuo chetu" alisema Hamisi mwanafunzi wa mwaka wa tatu na kuongeza kuwa; "Harufu ya wizi inanuka hapa chuoni tunalazimishwa kulipa direct costs kubwa sana tofauti na miaka ya nyuma"

Wanafunzi hao waliendelea kusema kuwa mwaka huu wa masomo 2010/2011 wanalazimishwa kulipa direct costs jumla ya shilingi Tshs. 88,000/= kwa mhura, tofauti na mwaka wa masomo uliopita ambapo walilipa jumla ya Tshs. 76000/=

Walisema kutokana na kauli ya uongozi wa chuo hicho UDOSO waliwataka wasilipe pesa hizo bali walipe kiasi cha Tshs.81,000/= ambapo walichanganua kuwa accomodation ni Tshs. 56,000/= pesa ya mtihani ni Tshs. 20,000/= na hela ya usajiri ni Tshs. 5,000/= jumla Tshs. 81,000/=, lakina pamoja na tamko la UDOSO uongozi wa chuo bado unakataa, jambo ambalo linawasikitisha wanafunzi hao.

Walisema chuo kinatakiwa kutoa maelezo ya kutosha ili kuwalizisha wanafunzi hao kwani bila maelezo ya kutosha wanaona kama wanaibiwa pesa zao, na ukizingatia wengi wao wanatoka katika familia masikini sana .

Sasa ndugu wanablogu wenzagu sasa tujadili kuhusu chuo hicho kuwa na utaratibu usioeleweka kwa wanafuzni. Je, dalili gani hasa? Je, ni utaratibu mzuri unafanya na chuo chetu  kikuu Afrika mashariki na kati? Tatizo liko wapi kwa uongozi wa chuo au? Nakaribisha maoni yenu bonyeza katika kisantuku kilichoandikwa toa maoni na utoe maoni yako yatasomwa na watanzania dunia nzima.

Monday, November 15, 2010

Jinsi ya Kumfanya Mwanamume Apagawe na Penzi Lako

LEO nimependa  kuongerea kuhusu  namna ya kudumisha penzi iwapo wewe umeolewa hasa kwa kina mama ambao penzi lao ninaelekea kuyeyuka. Na bila jitihada za hapa na pale penzi lako na mumeo linaweza kunyauka kabisa!!! Na ukumbuke wahenga walisema PENZI ni MAUA kuna kuchanua na kunyauka. Na penzi linaponyauka huwa yanatokea maumivu makali sana ndani ya moyo, maumivu ambayo hayana kifani. Sasa ufanye nini ili penzi lako lisinyauke? Zingatia yafatayo:

i) Hakikisha unakuwa karibu na mumeo
ii) Mumeo akirudi kutoka safarini au kazini mupokee kwwa mabusu na upendo wa hali ya juu
iii) Kama utakuwa na nafasi jitahidi kumuandikia msg mumeo za upendo na kumfariji
iv) Na mwisho kumbuka kuwa munapokuwa katika sita kwa sita jitahidi kutoa sauti ya mahaba huku ukijitahidi sana kumpa penzi kutumia ujanja wako, na kama atamaliza mwambie "POLE MUME WANGU"

.
Kwa leo ninakomea hapo kumbuka kuwa wanaume ni watu wa kujaliwa kila wakati na kubembelezwa Mwanasaikolojia wa mapenzi Dr. Linda wa chuo kikuuu cha Oxford aliwahi kunena ya kwamba hakuna dawa ya mapenzi zaidi ya kuonyesha upendo kwa umupendae.

Saturday, November 13, 2010

THE WORD RELATIONSHIPS

Relationships move beyond friendship. They occur when two people feel emotionally attached, fulfill each other’s needs and generally feel interdependent. When a true relationship exists, several components are present:

Trust; relationships must be built on a foundation of trust. We need to be to count on others and feel that they will be open with us.
Honesty; no relationship can survive if the partner are no honest with one another. Each partner must share a commitment of truth. Those in good relationships accept one another, blemishes and all. A relationship based on untruths or even half-truths lacks depth and meaning.

Mutual support; healthy relationships are characterized by mutual support. A partner’s well-being should have an impact on you, and your well-being should affect your partner. In best way the partner seek out what is best for both, and they act as advocates for and defend each other.

Loyalty; the mark of a good relationship is loyalty. Loyalty implies the relationship partners are supportive of each other, even in times of adversity and difficulty.
Acceptance; your best friend develops a love for the Dave Mathews band and listens to their CDs seemingly without interruption. You can’t stand listen to them. Do you decide that you can no longer be friends? Of course not.

BULDING LASTING RELATIONSHIPS

Few of us we lead our lives isolation. There’s reason for this: relationships with others a critical aspect of our sense of well-being. The support of friends and relatives helps us feel good about ourselves. In fact studies have found that our physical and psychological health may suffer without friendships. The social support of others acts a guard against stress and illness. And if we do get sick, we recover more quickly if we have a supportive network of friends.

“I have met the most amazing individuals and made the most incredible friends in such a short amount of time” Said Lenny UDOM University student

Although some of us making friend is ease, for others making friends is some difficult. But building relationships is not a mystery. Here are several ways to go about it.

Invest time with others; there is no better way to demonstrate that you are interesting in friends than investing time. You can expect friendships to flourish unless you spend time with people.

Reveal yourself; good friends understand each other. The best way to make that happen is to let others get to know you. Talk about where you come from, what is your family like. Find out about the other person. Having deeply understanding about where someone comes from not only helps to build bridges between people of different racial and ethnic backgrounds but it also helps build friendships. By honestly communicating your beliefs and altitudes, you give others the chance to learn those things you have in common.

Let other know you like them; it seems scary, but don’t be coy and try to pretend you are uninterested in the friendships of others. Take the risk of being rebuffed. You don’t have to announce outright that you like someone. Instead reveal you interest in a friendship by inviting the person to do something with you or simple by engaging in conversation, sharing something about your life. Your actions will speak louder than word

Accept others as they are; not as you would like them to be; one mark of friend is to acceptance of people the way they are, warts and all, and not way would like them to be. Do not impose conditions on accepting others. Keep in mind that no one is perfect and that everyone has both good and bad qualities.
Show concern and caring; this is really the substance of friendship and the basis for the trust that develops between friends. Don’t be afraid to show your interest in the fortunes of others and to share the sadness then they share some setback or loss.

Not everyone make a good friend; people who put you down, consistently make you feel bad, or behave in ways that violate your own personal standards are not friends. Choose your friends based on the good feelings you have when you are with them and the concern and caring they show for you. Friendship is a two way street.

Friday, November 12, 2010

The Ways That Make Success in Life & Education


ORGANIZE
By determining where you want to go and expressing your goals in terms that can be measured, you have already made a lot of progress. You might thing you’re now ready to head out and begin the intellectual trip to student success. Consider the tools for studying

WORK
You’re ready. Preliminaries are out of the way. You’ve prepared and you’ve organized. Now its time to get started actually doing the work. In this consider the following:

•Effort is the causes of success

•Be response to your failures; when you do poorly don’t blame the teacher, text books, or job that keep away from studying.

•Think positively, assume that the strength that you have will allow you to succeed and that and if you have problems you can figure out what to do.

•Accept that you can’t control every thing; think things that can be changed and those can’t.



EVALUATE
In this you should do an evaluation of your work, and after that you should do the following:

•Take a moment to congratulate yourself and feel some satisfaction. If you have done the work according to reach your goals or at least to the point of reaching goal just congratulate yourself.

•Compare what you’ve accomplished with the goals you’re seeking to achieve. Think back to the goals, both short-term and long-term that you are seeking to achieve.

•Evaluate what you’ve done if you were your current instructor. Now exchange body and mind again. This time, consider what you’re doing from the perspective of the instructor w ho gave you the assignment. How would he/she react to what you have done?

•Be fair to yourself; the guidelines for evaluation will help you to determine just how further work is necessary and, even more important, what work is important?

•Based on your evaluation, revise your work; if you’re honest with yourself it’s unlikely that your first work will satisfy you. So go back to work and revise to what you have done.

RETHINK
Rethink what you have accomplished earlier means to bring a fresh eye to what you have done. It involves critical thinking that involves reanalyzing, questioning and challenging our underlying assumptions.

Strategies for Success in College and Life

Dear Student,

Do you find that there’s not enough time t o accomplish all the things you want to do? Do you put off studying for tests until the last minute? Do you sometimes have trouble making decisions?

If so you’re not alone. Every first year college student encounters challenges such as these, and many others. That’s where Psychology Blog brings to learning strategies for success in colleges and life come in it. It is designed to help you master the challenges you will face in college and in you are everyday life. The over learning system which is based on five key steps embodied in word POWER (Prepare, Organize, Work, Evaluate and Rethink). These teach strategies that will help you to become a more successful student and that will give you an edge in attaining what you want to accomplish in your life.

But it’s up to you to make use of this blog. By familiarizing yourself with its features and using the built-in learning aids, you’ll maximize its usefulness and be more likely to get the most out of it.

Friday, April 9, 2010

Je utajisikiaje kama mpenzi wako atakuambia sina cha kukupa ila nakupa hili pendo mpz?

I Give This Love to You

By Lutonja Fita

I give this love to you
Since I have nothing to give you
Keep it like heart
When night comes to cove you
The winter can bite through NOT
I love you dear Subira.

I have nothing else to give you
So it is only love full of valentine
That no one can count
I say no one can count
It is only you to count
I love you dear Subira.

I have nothing else to give you
Only warmly love dear
To warm your body like arm
To warm your skin in huge dream
Like train passing Mwanza to DSM
I love you dear subira.

Keep it like treasures
Life become sweet in night dreams
Sweet as Azam ice creams
Sweet as juice Zam Zam
That made in Dar es Salaam
I love you dear Subira.

Warm yourself with this love let
Love originated to my heart
Don’t move to any cold hut
Rest in this feels safety
Warmly love like coat
I love you dear Subira.

It’s all dear to give you
Since I have nothing else to give
Only enough for you is love
Even God emphases love
Adam and Eve shared love
I love you dear Subira,

Thursday, March 25, 2010

Utajitambuje Kama Unaakili???????????????????????


KWA mujibu wa Mwanasaikolojia mwenzangu Howard Gardiner aliandika kuwa binadamu wanatofautiana kiakili kila binadamu anauwezo wake katika kufikiri.

Sasa ndugu mpenzi wa blogu hii, utajitambuaje kuwa wewe unaakili kiasi gani? Wewe na wenzako munatofautiaje katika kufikiri? Kulingana na akili uliyonayo unatakiwa uwe nani na uishije katika dunia hii?

Jibu la maswali hapo juu ni kwamba ili kujitambua akili yako unatakiwa kuwafanya mahesabu ya akili yako. Na kwa mujibu wa Gardiner unatakiwa kufuata fomula hii hapa chini:

Chukua Akili ya Umri wako gawanya kwa Mtiririko wa Umri wako na Zidisha kwa Miamoja = Akili yako.

Akili= Mental Age (MA)            x    100
          Chronological Age (CA)

Kama mental age ni kubwa kuliko chronogical age jua kuwa akili yako iko juu zaidi ya kawaida, kama mental age iko sawa na chronological age jua kuwa akili yako ipo katika hali ya kawada na kama mental age iko chini ya chronological age jua kuwa akili yako iko chini ya kawaida.

Sasa jitambue wewe uko katika hali gani jifanyie uchunguzi ili kujitambua zaidi fanya mahesabu ya kujua akili yako ili uweze kujikonturo na maisha, jiwekee malengo kwa kufuatana na uwezo wako wa kufikiri. Ni hayo tu mpenzi wa blogu hii na kama unapenda zaidi kujifunza juu ya habari hii bonyeza katika kifungu cha kuchangia maoni na acha maelezo yako hakika nitayafanyia kazi.Zaidi kujitambua ni muhimu katika maisha yako

Sunday, March 21, 2010

Penzi ni Tamu Sana Jaribu Uone???



PENZI ni tamu sana kila mtu anatambua hilo, na kukoswa pendo ni uchungu sana katika maisha ya binadamu.

Pamoja na hayo yawezekana wewe unayesoma blogu hii na wewe unampango wa kumuacha mpenzi wako, kutokana na sababu mbalimbali lakini yote hayo ni sawa na kupotea ndugu yangu.

Nakuomba sana usimuache mke wako kwani daima ulishamutamkia kuwa unampenda na hutamuacha kamwe katika maisha yako! Kumbuka baada ya kumuacha mrembo bibie utapata nini au utafaidika na nini? Zaidi ya kuanza kujuta na kuumia roho yako?

Wapo wanaume wengi wanaoachana na wake zao matokeo yake wanaanza kujutia kitendo hicho.

Namkumbuka baba mmoja tajiri mkubwa katika jiji hili la Dar aliwahi kuja katika ofisi zetu za ushari ili kuomba ushari wa doa yake
Baada ya mke wake kuchoshwa na baba huyo na kuamua kurudi kwao Mwanza.

Sasa baada ya kuachwa baba huyo alianza kuumia zaidi na kuwa anashinda nyumbani badala ya kwenda kazini, jambo ambalo lilimpelekea kuja ofini kwetu kuomba ushauri wa kufanya ili mke wake arudi.
Nasi tulimpatia ushauri na tukamuita mke wake naye tukamupa ushauri wa umuhimu wa mke na mume katika ndoa, jambo ambalo liliwaunganisha na mpaka sasa wanaishi kwa amani na upendo wa ajabu.

Sasa ndugu yangu kumbuka kuwa mwanamke ni muhimu sana katika maisha yako, mwanaume ameumbwa kwa ajili ya mwanamke na mwanamke kwa ajili ya mwanaume sasa kunahaja gani ya kumtukana mke wako ambaye ni mzuri? Kunahaja gani ya kumfukuza mke wako anaye kupa penzi la dhati? Na kunahaja gani ya kuwa na msongo wa wawazo kisa mke wako mwenye penzi tamu kaondoka? Sasa mwambie mke wako nakupenda sana mke wangu na sitakuacha kamweeeee.

Jitambue

BINADAMU tumezaliwa kuwaza kila wakati Mwanasaikolojia Alfred Binett mtaalamu wa mambo ya Intelligent Quotients (IQ) alisema kuwa ndani ya dakika moja binadamu huwa anawaza mambo mengi sana.

Kwa hiyo ili kufikia malengo na mikakati ya maisha yako unatakiwa kujitambua uko katika sehemu ipi hasa unapowaza mikakati ya maisha yako.

Usikubali kuyapa nafasi kubwa mawazo yasiyokuwa na manufaa katika maisha yako jitahidi kuyatupilia mbali na kukubaliana na mawazo ambayo yatakuletea manufaa, amini kuwa hujazaliwa masikini bali umezaliwa kuishi kutokana na unavyotaka.

Kumbuka kuwa mikakati ya mawazo yako ndiyo yatakufanya ufikie malengo, anza sasa kuwaza mafanikio hakika utaona.

DIGITAL MEDIA PRODUCTIONS LTD

Watengenezaji wa vitambulisho, business cards, matangazo mbalimbali ikiwa pamoja na kupiga photocopy, kuprint vipeperushi, vitabu, magazeti, majarida ya kila aina sasa wamekupunguzia bei.

Kwanini uhangaike? wakati DMPL wapo kwa ajili yako, lete kazi yako sasa tutaitengeneza kwa kiwango cha hali ya juu.

Kwa maelezo zaidi fika chuo kikuu cha Dodoma block “F” chumba nambari 74 au wasiliana nasi kwa simu: 0764 992264, 0719 020253 au tuandikie: 1982leonard@live.com




LAPTOP INAUZWA

Laptop yenye rangi ya silver, speed processor 1.735, Pentium M, screen kubwa inahali nzuri inauzwa kwa bei poa. Kama unahitaji kwa shughuli zako mbalimbali wasiliana kwa simu 0719 020253, 0764 992264.

Tangazo be the partnerof profits

BLOGU yako ya Saikolojia bado inakaribisha matangazo kwa wale wote wanaotaka kutangaza biashara zao kupitia mtandao huu unaangaliwa dunia nzima.

Kumbuka kuwa biashara ni matangazo, tangaza biashara yako upate faida zaidi na zaidi hakika mtandao wa Saikolojia unalipa zaidi.

Kwa maelezo zaidi wasiliana nasi kwa simu: 0764 992264 au 0719 020253 kwa e-mail: fitazi@hotmail.com



PSYCHOLOGY blog now welcome you to advertise your business on this blog which is viewed by all people around the world.

Remember that business is a partner of ADVERTS, make more profits through advertisings & remember that Psychology blog pays.

For more information contact us: +255 764 992264, +255 719 020253, e-mail: fitazi@hotmail.com

Friday, January 22, 2010

Uchumba na Marafiki

KUTOKANA na blogu hii kuwa ni mojawapo ya kivutio kwa watu mbalimbali dunia, baachi ya wadau wa wamependekeza kuwepo na nafasi za watu kujitokeza na kutafuta wachumba na marafiki. Wafuatao wanatafuta wachumba na marafiki:
Anaitwa Asha Hamis jinsia mwanamke anasoma chuo kikuu cha Dodoma, umri wake ni miaka (23) ,mrefu wa wasitani, rangi yake ya maji ya kunde, msafi na anapenda kuolewa, amejitokeza katika safu hii ya blogu akitafuta mchumba ambaye atakuja kuwa mume wake kipenzi cha moyo. Habagui kabila wala dini bali anachohitaji ni mwanaume. Kama yupo ambaye ameguswa naye awasiliane naye kwa namba 0719 030354
Pia naye Subira Juma wa Tanga, umri miaka 43, jinsia mwanamke, kazi ni mfanyabiasha wa bidhaa za magari, naye amejitkeza kupitia E-mail ya blogu hii ambayo ni: fitazi@hotmail.com akitafuta mume wa kumuoa ambaye anaumri wa kuanzia miaka 23 hadi 60. Kama yupo mwanaume huyo awasiliane naye kwa namba 0787 183736
Kama unatafuta mchumba,rafiki, mke mume au unataka ushauri wa kidoa, unahitaji maisha ya furaha siku zote, Andika shida yako na utume kupitia E-mail ya blogu hii: fitazi@hotmail.com au wasiliana nasi kwa simu namba: 0764 992264. Usihangaike tuma sasa hivi.

Thursday, May 21, 2009

Penzi la Wahindi

KARIBU tena ndugu zangu leo napenda kujua zaidi kuhusiana na mwananke wa kihidi na wakiafrika nani mzuri zaidi na nani anahusudu mapenzi kuliko. Kwani kumekuwepo na mkanganyiko wengine wanasema wahindi wanabaridi sana wengine wanasema waafirika wanajoto sana je, ni kweli? Wengine wafrika ni wazuri wengine wahindi ni wazuri. Sasa tujadili kupitia maoni yenu.

Mwingine anapenda wachaga wengine wasukuma


BINADAMU wote ni sawa lakini tunatofautiana kimawazo, fikra, kiutendaji, kipawa nk. Haya nilikuja kuyadhitisha katika kufuatilia fikra za Mwanafalsafa aliyekuwa maarufu sana kwa uchambuzi wa fikra na mawazo ambaye alikuwa anaitwa Plato.
Katika kazi yake ya "Republic" Plato alisema kuwa kila binadamu ameubwa tofauti kutokana na wengine kuwa na akili nyingi ambaye yeye aliwaita "golden boy" ambao yeye hawa aliwaelezea kuwa ni wale wanaweza kuwa viongozi wa nchi yaani (Philosphers, Gvern Planners and Rulers)

Wengine wanaakili ya kawaida "Silver boy" kwa mujibu wa Plato hawa ni wale wanaotakiwa kuwa walinzi wa nchi yaani askali jeshi na polisi pia alisema kundi la mwisho wa wale ambao wanaakili finyu "Iron Boy "hawa Plato alisema kuwa kwa kuwa wanauwezo mdogo wa kupambanua mambo kazi yao ni kulima na kuwa wazalishaji wa bidhaa za nchi.

Hii ilikuja pale nilipojaribu kufanya uchunguzi wangu na kugundua kuwa kumbe hata katika suala la upendo binadamu tuko tofauti wengine wanapenda wanene wengine wembamba na wengine weupe wengine weusi.

Katika makabira wengine wanapenda kabira fulani, kama mimi ninapenda wachaga na wengine hawapendi wachaga wengine wasomi wengine hawapendi wasiomi kwahiyo kutokana na hili binadamu tuko tofauti.

Je, katika mtazamo wako wewe unaona je? tujadili.

Wednesday, May 20, 2009

Mwanafalsafa Socrates alihusudu ndoa


SIKU moja nilikuwa naelekea kwenye press conference moja tukiwa na rafiki yangu ambaye ni mwanahabari mwenzangu tulipofika maeneo ya Magomeni akaniambia kuwa anataka kuoa nami nikatafakari kwa kina maelezo kisha nikamjibu kuwa ni jambo jema kuoa kwani kuwa na mke ni mojawapo ya maisha tuliopangiwa na Mungu.


Mara nikakumbuka usemi wa Mwanafalsafa wa Kigiriki aitwaye Socrates naye alidhamini sana ndoa kwani aliwahi kusisitiza kuwa kama ukiona maisha ni magumu ni vizuri kuoa mwanamke Mzuri. "If you see life is hard you have to find a good wife to refresh your mind" alisema Socrates.


Jambo la kuwa na Mwanamke ni mhimu sana kwani watu wengi hasa katika nchi zinazoendelea huwa wanapata msongo wa mawazo kutokana na maisha kuwa magumu lakini Mwanasayansi Samuel Spire anasema kuwa kuwa na Mwanamke ni mojwapo ya kupunguza msongo huo wa mawazo.


Anasema kuwa mwanamke anasaidia kuondoa msogo wa mawazo kwa mwanaume vilevile mwanaume anasaidia kuondoa msongo wa mawazo kwa mwanamke. Hii inatokana na homoni zinazotolewa pindi mwanaume au mwanake anapokuwa na mpenzi wake.


Je , wewe ndungu yangu ulishawahi kukutana na msongo wa mawazo baadaye ulipomuona mpenzi wako ukajisikia uko fresh? sasa tujadili katika kibaradha chetu.

Sunday, May 17, 2009

Falsafa na Penzi


NIMERUDI tena ndugu zangu nilikuwa masomoni kwa muda kidogo ila sasa hivi niko kazini kwangu ninachati na mhariri wangu wa habari ambaye ndiye Mwalimu wangu Mkuu katika kuhakikisha jamii inaelimika kupitia vyombo mbalimbali vya habari.
Huko masomoni nimejifunza mambo mengi sana nimejifunza kuwa kumbe watanzania waliowengi hawajui kingereza!!!! Nilishaangaa sana Mhadhiri wangu wa lugha aliponiambia hata Kenya hawajui kingereza!!
Kwa sababu fani yangu ni Kudadisi nilimhoji kwa nini anasema hivyo ? Jibu alilonipa Ahhh!!! eti katika vitabu alivyosoma hakuna sehemu ambayo amekuta kumeandikwa rafudhi ya kingereza ya Afrika Mashariki!!(East African Accent) hayo yote nimejifunza kwa sababu nilikuwa nafuatilia kwa ukaribu sana mongozi wa lugha hii ya kingereza.
Ama kweli elmu haina Mwisho kwani nilijifunza mengi sana? Ikiwa pamoja na Mhadhiri wangu wa Falsafa alinifundisha kuwa elimu haina Mwisho huku akisema elimu inaanzia mtu anapozaliwa na pale anapokufa!!. Kwasababu napenda Falsafa niliamua kuziunganisha falsafa za Mhadhiri wangu na kuzifanyia kazi.
Jambo nililogundua ni kwamba hata penzi halina mwisho pendo linadumu siku zote ila kunakumchukia mtu fulani, lakini pia ukimchukia huyu utampenda huyu ndiyo maisha ya binadamu. Je kama tusingekuwa na upendo tungeishije katika dunia hii? Sasa tujadiliane ndugu zangu.




Tuesday, February 17, 2009

Maswali

NILIKUWA nimekabiliwa na majukumu mengi sana paka ilinipelekea kuwa nashinda njaa bila kunywa hata kahawa yetu ya kila siku ila sasa nimesimama tena ili kuweza kutafuna sawasawa hiki chakula chetu cha kila siku (kublogu) ila leo nitakuja na maswali ambayo yananiumiza kichwa kila siku.

1) Kupenda ni nini? na nini maana ya kupenda?
2)Ikiishi bila kuoa au kuolewa kuna hasara gani?
3)Kufanya tendo la ndoa maana yake nini?
4)Uzuri ni nini na ubaya ni nini?
5) Roho nzuri ni nini?

Haya ni hayo tu ndugu zangu ninaumia kichwa sana kutafakari juu ya maana ya maswali hayo ila nawaombeni tuchangie mambo haya katika kuyapatia maana yake. Amani kwako Markus, dada Yasinta, dada Koero, Fadhy na wengine wote na natumai tuko pamoja daima.

Saturday, January 3, 2009

Nilimpenda kwa sababu....?

KATIKA kumpenda mtu huwa kunachangiwa na vitu vingi sana kwa sababu binadamu tunatofautiana kifikra, kimaumbile, kimutazamo, kiuelewa, kihisia n.k. ambayo yote haya katika mapenzi huchangia mwamsho (feelings) wa mwili.

Kutokana vitu vyote hivyo binadamu anaweza kumpenda mtu mweusi, mweupa, mfupi, mwembamba, mnene nk.


Kuna watu wanapenda kuwa na wapenzi wembamba yaani watu hawa wakiona mwanamke/mwanaume mwembamba huwa wanapata hisia kubwa sana ya kumpenda na kutamani kufanya nae mapenzi ili walidhike kuwa wamehondomola kifaa ambacho wanakipenda sana.
Wengine wakiwaona mtu mnene hupata mwamsho wa kutaka kumuhondomola ili kulidhika kuwa wamefanya na mtu ambaye ni mzuri. Si mapenzi hata kuoa kunatokana na sababu hizo za kupata hisia ya yule umpendae hasa kukuvutia kwa jinsi alivyo.
Mwanasaikolojia na Mchungaji, Hoven Michal wa chuo kikuu cha Wheaton School of Thelogy katika jimbo la texas nchini Marekani alibainisha katika utafiti wake juu ya hisia kwa binadamu aliuandikia kitabu ambacho alikiita kwa jina la "Feeligs & Love" ya kwamba matendo ya mahaba kwa binadamu yanatawaliwa na hisia hasa kwa yule anayekuvuti.

Naye Fredy Hasin wa Dar es Salaam aliwahi kusimulia kuwa alimpenda sana mama Suzy (mke wake) na alikuwa anamhondomola vizuri sana wakati wa chakula cha usiku lakini alikuja kumchukia kutokana na kunenepa ghafra jambo ambalo alikuwa halitaki katika maisha yake.

Pia Maganga Magembe ambaye ni askali polisi wa kituo kidogo cha Nyakato aliwahi kuahadithia kuwa yeye anapenda wanawake wanene kwa sababu huwa anapata nafasi nzuri ya kufaidi tunda tamu wakati wa chakula cha usiku, jambo ambalo linampelekea kujiona fahari katika dunia ya maopenzi.

Sayuni Mahina alipohojiwa na Mwandishi Huria wa blogu hii alidhibitisha kuwa yeye mme wake ni Mwembamba na anapenda wanaume wa aina hiyo kwa sababu huwa wanamhondomola vizuri sana na kumfanya ajisikie utamu hadi kwenye kichwa. "Utamu huu ambao huwa naupata sijawahi kuupata sijui Mungu aliutoa wapi?" alihoji mama huyo.

Je, Mpenzi wa blogu hii wewe unapenda wako penzi wa aina gani? Sasa tujadiliane mada hii niliwahi kudika kipindi cha nyuma.

Friday, January 2, 2009

Nimefurahi sana


Haya ndugu zangu napenda kuwaarifu kitu ambacho ninataka kukifanya kwa sasa hivi. Kitu hicho ni kwamba nataka kwenda kusoma chuo kwani wahenga walituambia ya kwamba "Elimu Haina Mwisho" na kitabu kitakatifu kinatuambia ya kuwa "Mshikeni Elimu Msimuache aende zake maana huyo ni uzima wetu" kwahiyo wanablogu wenzangu nataka niendelee kufuata haya maandiko ili nione kama yanaukweli.


Ila ninatumai tuko pamoja popote nitakapokuwa, Bwaya, Markus mpangala, Dada Yasinta, Da Koero, na wengine Mungu awabariki sana.

Sunday, December 28, 2008

Utamu wa mapenzi unafanana na nini?

BILA shaka msomaji wa blogu hii unampenda sana wako kipenzi na yawezekana unafanya kama huyo hapo kwenye picha anavyofanya kuonyesha kuwa mnapendana sana, na ikifika wakati wa chakula cha usiku unabonyeza/ unabonyezwa vizuri tu na unasugua kwa uraini huku utamu wa mpenzi wako unausikia vizuri.

Ebu fikiria iwapo inatokea siku moja, mpenzi wako akakusaliti na kwenda kumpa chakula cha usiku mtu mweingine utajisikiaje? au itokee siku mpenzi wako akaamua kukuacha na kwenda kuolewa na mtu mwingine.

Fikria maumivu utayoyapata ni ya aina gani? Hakika penzi ni tamu kwelikweli hasa kwa yule anayempenda kwa moyo wote. Sasa tujadiliane unasemaje?

Penzi linahitaji uvumilivu


WAKATI mwingine huwa unajisikia kumchoka mpenzi wako, kuchukua jukumu la kumuacha wako mpenzi, kumkaripia wako mpenzi, kumuona kama anakasoro fulani hivi, kumuona hakufai au hafai kuishi na wewe ikiwa pamoja na kutamani kuoa au kutafuta mwingine mpenzi.


Yote haya mambo huwa yanatokea kwa binadamu wa jinsia zote. Sasa nakuuliza kwanini unafikia hatua ya kufanya mambo kama hayo? Kama kweli uliamua kumpenda mpenzi wako ya nini tena kumchukia na kumuona hakufai?


Watalaam wa masuala ya mapenzi wanabainisha kuwa kumchukia mpenzi kunasababishwa na vitu vingi sana, ambapo mwanasaikolojia na mtaalam wa masuala ya love Haliet Julliu alifafanua katika kitabu chake cha "Bad Love - 2008" kuwa jambo la kwanza ambalo linamfanya mpenzi wako kukuchukia ni:


i)Uchufu wa mwili wako pia unapokuwa mchafu ndio unaongeza hatari ya kuchukiwa na mpenzi wako.


ii)Uchafu wa nyumba au chumba ambacho unakaa na mpenzi wako hasa hili linawahusu mwanawake, jambo hili huwa linawakera wanaume.


iii) Kupata mpenzi nje ya ndoa pia kunachakia mpenzi wako kukuchoka na kukuona hufai kisa kapata wa kumhodomola hasa akimpata anayejua mapenzi.


iv) Wewe mwenyewe kuwa mkali pindi unapomuona mpenzi wako nako kunachangia kumfanya atafute mwingine ambaye ni mpole ili apate kuliwazika zaidi kimahaba na,


v) Kuwa na wasiwasi wa kusalitiwa na mpenzi wako jambo ambalo huwa linazua mitafaruku kwa wapenzi na kusababisha kuchukizana na pengine kupelekea kuachana kabisa.


Kwahiyo nawashauri sana ndugu zangu mjitahidi kuepuka mambo kama haya ili kudumisha penzi zaidi.Sasa tujadiliane kuhusu suala hili na pia napenda kuuliza Je, penzi ni nini?






Saturday, December 27, 2008

Mavazi ni mojwapo ya kuvutia penzi


Ndugu ili upendwe unatakiwa kuwa mbunifu wa mavazi yako, uanatakiwa kutambua mavazi ambayo yanamfurahisha mpenzi wako, jambo hilo linatia hamasa ya mpenzi wako kuvuta hisia hata kama anakuhondomola, akikumbuka unavyovaa nguo zako na kukufiti anapata hamasa zaidi ya kukushughulikia ipasavyo.
Katika tafiti mbalimbali za wataalamu wa mapenzi wanafafanua kuwa binadamu akiwa anafanya mapenzi huwa fikra zake zinatawaliwa na kumfikiria mpenzi wake. Jambo hili humpelekea kupata hisia kali za kumkubuka jinsi anavyomjari, anavyovaa, anavyojituma, anavyoongea, sauti yeke jinsi ilivyotamu yote haya huwa yanaingia katika fikra za wapendanao wakati wakiwa wanakulana au kuhondomolana jambo ambali pia huwafanya wanamaliza mapema, pia humusababisha mwanamke kutoa kilio cha utamu anaoupata kwenye fikra zake, na mwanaume anaweza kutoa milio pia ya kusikia utamu unazidi jinsi anavyohondomola na kupata hisia kali za mpenzi wake.

Tabasamu uhamasisha Ngono

Je, unapokuwa na mpenzi wako huwa unatabasamu? au unanuna kama unakamuliwa jibu? kumbuka kuwa kununa kunasababisha mpenzi wako akuchoke mapema zaidi au kukuacha kabisa. Nakushauri kuanzia sasa hivi jitahidi sana kuwa unatabasamu kila wakati kwani binadamu tumeumbwa na upendo kwa kila mtu, japo kama utajua jinsi ya kumfanya mpenzi wako akupende. Katika dunia hii hakuna dawa ya mapenzi bali dawa ya mapenzi unayo wewe mwenyewe. Kuwa makini utaacha watafuatwa wanaojua kupenda na kuhondomola.

Kwanini penzi unanitesa kiasi hicho.

Penzi ni kipofu. Penzi linatesa sana. Kwanini penzi linatesa? Mtaalam wa masuala ya mapenzi Pinig Huing wa china alibainisha kuwa penzi ni tamu kuzidi kila kitu hapa duniani na kuongeza kueleza kuwa penzi pia linaumiza sana.


Hii ni kweli kabisa ndugu yangu yakupasa kuanzia sasa hivi utambue kuwa penzi ni tamu ukijua hilo ninaimani utamdhamini mpenzi wako na utampenda zaidi. Ili kuhakikisha unamjali mpenzi wako yakupasa uonyeshe upendo kila unapokuwa na mpenzi wako.


Katika dunia ya wapendanao unatakiwa kumjali dear wa moyo wako ili ajui kuwa unamjali jambo ambalo litawafanya muishi kwa furaha na raha za dunia kuziona. Hupaswi kuona kwa mwenzako jinsi anavyomjali dear wake halafu na wewe uanze kumjali mpenzi wako.


Katika vitu vya kuzingatia katika kumuonyesha mpenzi wako unamjali ni kumbusu kila wakati, kumkumbatia kila wakati, kumhondomola ipasavyo huku ukitumia kila staili za kuhondomola, hapo utakuwa umemjali mamsapu wako ipasavyo na jambo hilo hatakusahau kamwe atakuwa anakukumbuka hata kama ukiwa kazini.

Zawadi ni chachu ya penzi


Nani alikuambia kuwa mtu ukimpa zawadi ya pipi utakuwa humpendi? nani alikuambia zawadi zenye thamani ndizo zinaonyesha ishara ya pendo?


Karlosia Hukou mwanasaikolojia wa nchini Korea aliwahi kuandika katika kitabu chake cha "Gift is Gift" mwaka 2006. Ambapo katika kutabu hicho alielezea kuhusu umuhimu wa zawadi kwa wapendanao.


Hukou alibainisha kuwa zawadi ni ishara ya upendo haijalishi zawadi ya thamani gani?, alieleza kuwa hata mpenzi wako ukimununulia nguo ya ndani kama anakupenda atazidi kukupenda zaidi.


Naye Sarah James wa Marekani aliwahi kubainisha katika tafiti (research) yake aliyoifa mwaka 2008 katika chuo cha Havard, alifafanua kuwa iwapo mpenzi wako utakuwa unamfanyia saplaisi ya kumnunulia zawadi ndogo ndogo kama pipi na kumpa huku ukimwambia "Mpenzi wangu pokea hii zawadi nimenunua kwa ajili yako dear" jambo kama hilo alisema linadumisha penzi.


Je, wewe unamununulia zawadi za aina gani mpenzi wago?

Monday, December 15, 2008

Nguvu ya penzi tumepewa na Mungu


Huwa ninajiuliza hivi penzi ni kitu gani? penzi lilitoka wapi? kwanini ukipenda kuzidi kiasi unakuwa kama kipofu? kwanini penzi linawafanya watu kubadilika? Kwanini penzi linaua yaani mtu anaamua kujiua kisa kakataliwa na mpenzi wake? Au anaamua kumuua mtu aliyemchukulia mpenzi wake?


Yote haya ni nguvu ya penzi ambalo tulipewa na Mungu kwakweli penzi ni kitu kitamu sana tena sana!! hakuna kitu cha muhimu katika dunia hii kama penzi.


Binadamu hata kama munapendana kiasi gani ukimchukulia mpenzi wake urafiki unaisha na munakosana kabisa ikiwezekana hata kufanyiana mambo mabaya. Hata baadhi ya wanyama ukiwakuta wanafanya mapenzi huwa wakali wanaweza kukurarua ukiwasogelea wakizani utawanyang'anya wapenzi wao.


Jamani penzi ni kitu gani? Kwanini penzi linakuwa hivyo?

Mwanaume anachelewa kurudi nyumbani


"Najitahidi sana kumshauru mme wangu Leonard ili awe anawahi kurudi ili nimufaidi mme wangu lakini hataki kutekeleza ushauri wangu sasa ngoja kuna siku nitaenda kumchongea kwa bosi wake ili afukuzwe kazi nifaidi penzi lake kwa kuwa naye masaa yote" alisema dada mmoja ambaye anafahamika kwa jina la Mariam Sabaganga mkazi wa Mwanza.


Pengine wa wewe unamawazo kama hayo kutokana na mme wako kutingwa na kazi nyingi na hatimaye kushindwa kuwa anawahi kurudi nyumbani mapema. Nakuomba usiwe na wivu kiasi hicho kwani kazi ya mme wako ndiyo inawafanya kuishi au kujiongezea kipato nyumbani kwenu.


"Ninajuta sana kutokana na watoto wetu kushindwa kusoma kutokana na mme wangu kufukuzwa kazi baada ya kumchongea kwa bosi wake kuwa anatabia ya kumuibia bosi pesa za kampuni yake na kuleta nyumbani na zingine kuweka benki" alisema mama Aisha mkazi wa Area "D" mjini Dodoma baada ya kujuta kutokana na kumsababishia mme wake kufukuzwa kazi kwa wivu wa mapenzi.


Aliendelea kusema kuwa "Kama ningejua kama tutateseka kiasi hiki, yaani tunalala njaa huku watoto hawaendi shule, kwakweli inaniuma sana na ninamuomba Mungu atusaidie angalau tupate pesa za kuwasomesha Aisha, Ben na Hamis!"alisikitika mama huyo.


Sasa je, na wewe unawivu wa kiasi hicho? Toa maoni yako ili kusaidia kufanikisha kwa utafiti ambao unafanya na shirika la Tanzania Women Reseach.

Kazi ya uandishi wa habari

NINAPOSEMA Mwandishi wa habari kwa maana nyingine ninamaanisha Mtangazaji, Sasa ndugu zangu wasomaji wa blogu yenu ya saikolojia tunaambiwa ya kwamba mtu ambaye anafanya kazi ya kutangaza anatakiwa kuwa makini sana katika kazi hiyo, akiendana na kuwa mbunifu wa jambo kila siku.

Sasa basi kuhusiana na jambo la mapenzi Mtanzaji wakati ukiwa ndani ya studio unatangaza kipindi chochote unatakiwa kuondoa fikra za migongano au mikasa ya mapenzi iliyokupata aidha kutoka kwa mpenzi wake au sehemu nyingine.

Mtaalam wa Masuala ya mapenzi ambapo pia ni Mtangazaji wa Classic Fm Evas Chris aliwahi kufanya utafiti na kukundua kuwa asilimia 96 ya watangazaji wanaopata misukosuko kutoka kwa wapenzi wao mara nyingi wanafanya vibaya katika vipindi kutokana na kufikiria misukosuko ya wapenzi wao.

Chris katika tafiti yake hiyo ambayo aliita kwa jina "Good Presenter Research" alibaini kuwa wanandoa wengi ambao walikuwa katika hali ya kukosana na wapenzi wao walifanya vibaya katika media.


"Nilimshauri Denis Jakky kila mara aachane na mke wake kutokana na mke huyo kumfanya amfikirie yeye hata wakati ikiwa anatangaza kitendo ambacho kilimfanya kushindwa kutangaza vizuri" alisema Jeff Jeakim Mtangazaji wa Mercy Fm iliyoko Texas USA.

Tabasamu ni nguvu ya penzi

IMEELEZWA kwamba mtu ambaye anatabasamu kila wakati huwa anaonekana mzuri na mtanashati kuzidi mtu ambaye saa zote yeye ni kununa tu. Wataalam mbalimbali wa masuala ya saikolojia wamefanya tafiti juu ya jambo hili na kubaini vitu kama hivyo.Wataalam kutoka Chuo Kikii cha Haverd nchini USA, walifanya utafiti na kubaini mtu ambaye ananuna kila wakati huwa anazeeka mapema na huonekana mbaya wa sura kutoka na sura yake kuzoea kujikunja.

Ikiwa naye Mtaalam wa Saikolojia ya Mapenzi Richard Athony wa Uingereza katika utafiti wake anasema "Wanawake wanaochukia ndoa zao wengi wanaoneka kama wazee kutokana na kutokuwa na raha Wanawake wanatakiwa kuzifurahia ndoa zao ili kuepuka kuzeeka mapema" alisema Mtafiti huyo na kuongeza kuwa: "Uzee huo unatokana na kukoswa raha kila wakati jambo ambalo linawasababisha kutokujijari ikiwemo kuoga vizuri na kujipodoa" Je wewe mfuatiliaji wa blogu yako ya saikolojia umefanya utafiti juu ya suala hili na umegundua kitu gani? Changia maoni yako.

Wednesday, December 10, 2008

Penzi la Kweli


Penzi la kweli ni lile la kuaminiana na kujaliana kwa kila jambo. Penzi la kweli halipimwi na utajiri. Penzi la kweli halipimwi na vigezo. Penzi la kweli halina mfupi na mrefu. Penzi la kweli halina Muzungu na Mwafrika. Bali penzi la kweli ni kupendana kutoka rohoni.

Ukiwa beach


Japo kama umetoka na mpenzi wako mkaenda ufukweni kupungwa upepo huku mukiinjoi maisha ya huko cha msingi hakikisheni munafanya mamboyenu bila kuogopana ili mkitoka pale kila mmoja amelizika na huduma ya mwenzake. Munatakiwa kkubebana na kubusiana kila mmoja na malov dav mengine.


Mtaalam mmoja wa mapenzi aliwahi kusema "kubadilisha mazingira kwa wapendanao husababisha upendo kuongeza" pia aliongeza kuwa "jambo hilo linasababisha kudumisha penzi na kuaminiana katika penzi"

Tuesday, December 9, 2008

wanawake wenye hips pana


Mtaalam wa saikolojia Prisca Janny alibainisha kuwa wanawake wenye hips kubwa ni wepesi sana wa kupata mimba tofauti na wanawake wenye hips nyembamba (milonjo) alielezea katika kitabu chake cha "Hips love" cha mwaka 2008 kuwa wanawake hao wenye hips kubwa wakilala na wanaume huwa ni rahisi sana kunaswa na mimba.


Pia nchini Uholazi Mtafiti wa masuala ya kizazi Christopher Bincom aliandika katika kitabu chake cha "Birth and Risk" cha mwaka 2004 kuwa wanawake wenye hips pana wanaweza kupata mima kwa haraka zaidi. Pia alifafanua kuwa wengi wa wanawake hao huwa wanazaa watoto wa jinsia ya kike kutokana na kuwa wengi wanawahi sana kufikia kilele ambapo wanasababisha maji mengi kujaa kwenye sehemu ya chakua cha usiku kwahiyo maji hayo yanasababisha mbegu za kiume Y kushindwa kupenya mpaka kwenye yai.


Alibainisha kuwa mbe za Kike X huwa zinaweza kuogerea kwenye maji mengi zaidi ya mbegu za kiume hiyo ndio maana zinapenya haraka mpaka kwenye yai kuliko mbegu za kiume Y.



Pozi linadumisha penzi

Ndugu yangu kumbuka kuwa pozi lako nalo ni chachu ya kudumisha penzi unatakiwa kukaa katika mapozi ya mvuto kwa mpenzi wako. Katika tafiti mbalimbali ikiwemo ya Mary Jackson zinabainisha kuwa wanawake wenye mapozi mengi wanapendwa na wanaume wengi zaidi ya wale ambao hawajui mapozi.

Naye Horaw Pierre wa ufarasa alifanya utafiti katika jiji la maraha kuzidi majiji yote duniani "Paris" na kubaini kuwa wanawake wengi wenye mapozi wanapendwa sana na wanaume lakini wengi wa wanawake hao wanaolewa lakini ni wepesi sana wa kuachika kutokana na fikra zao za kujihisi kuwa wao ni wazuri na kufanya kiburi kwa waume zao. Pia naye Ching Annig wa china alibainisha katika utafiti wake kuwa lisha ya kupedwa na wanaume wengi pia wanawake hao wenye mapozi ni wataalam sana wa kula chakula cha usiku kuliko wale ambao hawana mapozi.


Je wewe mfuatiliaji wa mblogu hii unasemaje juu ya suala hili ni kweli wanawake wenye mapozi wanapendwa na wanume zaidi ya wale ambao hawana mapozi?

Penzi halina Mzee


Nani alikuambia kuwa mzee hapendwi na vijana? nani alikuambia kuwa mzee hajui kuhondomola? nani alikuambia kuwa mzee hajui kuonyesha penzi la kweli? Katika dunia hii penzi ni kitu kizuri sana.


Kuna watu wengine wanasema mimi siwezi kuolewa na mzeee? na wengine mimi siwezi kuoa mtu ambaye ananizidi umri yote hayo ya nini? kwani penzi linazeeka? Penzi daima si la mzee wala kijana peke yake bali penzi ni la wote.


Kuna rafiki yangu mmoja wa kiume anahela za kawaida tu, na ana gari moja alinunuliwa na mpenzi wake, huyo rafiki yangu aliwahi kuniambia yeye habagui cha mwanamke mzee au msichana anachojali ni yule ambaye ana hela tu. Nilishanga sana nikajua rafiki yangu hana penzi la kweli kwa wanawake.


Ndugu kitu cha msingi ambacho ninataka nikueleze ni kwamba kama wewe umetokea kumpenda mtu ambaye ni mkubwa kuzidi wewe usimuache kwa kisingizio cha ukubwa bali uangaliwe penzi la kweli kama unampenda na yeye pia anakupenda basi yawapasa muoane na penzi lenu litadumu kwa sababu mnapendo la rohoni.

Usingizi wa Penzi la Kweli hudumiaha penzi.


Mpenzi mfuatiliaji wa blogu yako ya saikolojia kumbuka kuwa penzi ni gharama ni lazima uligharamie ili uweze kulifaidi vizuri. Kwahiyo kumbuka kuwa hata wakati mlalapo na mpezi wako unatakiwa kuonyesha kuwa unampenda zaidi katika dunia hii, kwahiyo unatakiwa kumjali wako mahabuba wakati wote kuanzia chakula cha usiku mpaka wakati mmelala.


Katika kumjali hivyo unatakiwa kumkumbatia mpenzi wako pindi munampomaliza kula chakula cha usiku na kumuuliza "umeridhika na chakula nilichokupa?" Kama atajibu ndio, basi mkumbatie ili mlale vizuri mpaka asubuhi usidiliki kumuacha , kwani wataalam wa mambo ya ma lov dav wanabainisha kuwa joto lampenzi wako akiamuka asubuhi hata kamaataenda kazini lazima atakuwa analihisi katika mwili wake na hiyo ndio itamusababisha akupende zaidi.

Lips za mdomo zinavuti kufanya mapenzi

Wataalam wa masuala ya mapenzi wanabainisha kuwa lips za mdomo zinahamasisha mapenzi, hii ni kutokana na tafiti mbalimbali za wanasaikolojia juu ya suala hilo. Mwanasaikolojia Leonard Charles wa Urusi katika tafiti yake aliyoifanya mwaka 1883 aligundua kuwa wanawake wenye lips kubwa wanahamasisha chakula cha usiku tofauti na wanawake wenye lips ndogo.

Mnamo mwaka 2007 naye Mwanasaikolojia Joseph Havas alibainisha ya kwamba wanawake wenye lips kubwa wanahamasisha mwanaume kuamua kumpiga denda mwanake huyo ambapo pia naye Suzzy katika utafiti wake juu ya suala hilo aliwafanya wake utafiti katika jimbo la Texas alibainisha kuwa wanawake wenye lips kubwa wanapendwa na wanaume zaidi ya wanawake wenye lips ndogo.


Mpenzi mfuatiliaji wa blogu hii je, wewe unapenda mwanamke wa aina gani kati ya hao? niandikee maoni ili kuweza kufanikisha utafiti ninaoufanya mimi hapa tanzania.

Sunday, November 23, 2008

Wanawake wembamba watalamu wa chakula cha usiku

Imebainishwa kuwa wanawake wengi wembamba ni watalamu wa mapenzi kuzidi wanawake wanene, hii inatokana na tafiti mbalimbali zilizofanya na watalamu wa masuala ya mapenzi kama wakina Leticia Jackson wa US, Prof. Benjamin James wa Ufaransa, Dr. Edward Huloww wa Uingereza, hawa watalamu katika tafiti zao walizofanya katika nchi mbalimbali zinaonyesha kuwa asilimia 85 ya wanawake wembamba wanajua staili nyingi za kuhondomolana wakati wa chakula cha usiku, na asilimia 15 ya wanawake wanene ndio wanaojua kula vizuri chakula cha usiku. Je wewe unasemaje kama umefanya tafiti zako niandikie utoe maoni yako.

Kuvaa Tai


Wanaume wanaovaa tai inabainishwa kuwa wengi wa wanaume hao ni watu walio na nidhamu kubwa na wanajiheshimu kwa kiasi fulani japo kuwa wapo wanaume wengine ambao wanavaa tai lakini hawajiheshimu. Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zilizofanya na wataalamu wa saikolojia duniani, zinaonyesha kuwa zaidi ya asilimia 80% ya wanaume wanaovaa tai ni wale walio na nidahumu ya hali ya juu na asilimia 20% tu ya wanaume ambao hawavai tai yaani wanavaa nguo mbalimbali yakiwemo mavazi kama jinsi, tisheti nk, ndio wale ambao hawana nidhamu.

Macho yanahamasisha Penzi


Kumbuka ya kweamba macho ni kiungo kizuri sana kwani kazi yake ni muhimu katika binadamu ambapo hasa tunayatumia katika kitendo cha kuona, ila kuna siri kubwa kama huijui leo hii mimi nakuambia ili uanze kuitumia sasa hivi.


Seri hiyo ni kwamba macho pia yanaweza kuhamasisha mapenzi au kumvutia mtu kutaka kufanya mapenzi na wewe, ukiyatumia vizuri hakika utaona mabadiliko kati yako na mpenzi wako. Tafadhali anza sasa hivi kuyatumia macho yako vizuri ili kumvutia mpenzi wako.

Kumbuka kuwa nywere zinaweza kuhamasisha mapenzi.


Ndugu mada hii inakusa wanawake, napenda kuwaambia ya kwamba kulingana na tafiti zilizofanya na wanazuoni mbalimbali akiwemo wakongwe wa masuala ya mapenzi kama wakina Dr. Leonard Mashindano, James Ngoye, Zuzzy Gurter na wengine. Tafiti hizo zinaonyesha kuwa nywere kwa mwanamke ni mhimu sana kwani ni mojawapo ya kivutio kikuu katika suala zima la malove dav hasa mwanaume wengi wanavutiwa sana na mwanamke ambaye anaseti nywere zake kwa staili nzuri.


Sasa hapo kazi kwako mpenzi mfuatiliaji wa blogu hii kumbuka kuwa kuaanzia sasa jitahidi kuseti mwere zako hata kama huna hela za kwenda salon siku hizi mitaani kuna salon nyingi tu za bei poa nenda katika hizo salon seti nyere zako hakika kama unampenzi utaona mabadiliko atakuwa anakupenda zaidi ya mwanzo kwani wanaume tunahusudu sana nywere.

Kunenepeana sana


Siku moja nilkuwa chuo na rafiki yangu wa kike beatrece tulikuwa tumekaa kwenya sehemu ya kupumuzikia baadaye akapita Mwanaume mmoja karibu na sisi shutukia rafiki yangu ananiambia "ebu! muangalie yule baba, yaani mimi sipendi kuolewa na wanaume wanene walio na kitambi" nami sikumuuliza kwa nini hapendi.


Ila nikaamua kufanya utafiti (reseach) juu ya jambo hilo mwishoni wa utafiti wangu kulikuwa ni asilimia 91% ya wanawake niliowafanyia utafiti walisema hawapendi kufanya mapenzi na wanaume wanene au kuolewa na wanaume hao, na asilimia 9% tu ya wanawake waliopenda kufanya mapenzi na wanaume wanene au kuolewa nao.


Baadaye tena niakaumua kuwafanyia utafiti wannaume ambao wanapenda wanawake wanene nikapata asilimia 62% ya wanaume walidai wanapenda wanawake wanene na asilimia 48% walidai wanapenda wanawake wembamba yaani model.


Ndugu mfuatiliaji wa blogu hii wewe uko upande gani ponyeza kwenye neno toa maoni halafu niandikie wewe unapenda wanawake/wanaume wa aina gani? kumbuka maoni yako ni mchango mkubwa sana katika kuendeleza utafiti huu. Asante.

Uso ni kivutio cha kila mtu


Ndugu zangu hasa wale wanaohusudu mapenzi kumbukeni ya kwamba uso wako ndio kivutio cha kwanza cha mpenzi wako, wataalamu wa mapenzi wanatuambia kuwa binadamu waliowengi huchagua wapenzi kwa kuangalia uso wake.


Hii ni dhahili kabisa kuwa kila mtu anapotaka kuwa na mpenzi wake cha kwanza kumvutia ni uso wake, harafu umbo la mwili linafuata. Sadiki ya kwamba umukute mwanamke au mwanaume ambaye uso wake umeharibika ila anaumbo zuri tu, halafu niambie kata wewe unatafuta mchumba utafanya nini?


Kwa kila mtu nina maana ya mwanaume na mwanamke wote mnatakiwa kujipamba kila wakati na kuvaa nguo zinazovutia kwa kila wakati, wengi wa wanaume hawapendi kutumia vipodozi iti wanadai kuwa vipodozi ni za wanawake! ahaa! nani kakuambia hivyo acha mambo ya kizamani wewe mwanaume podoa mwili wako ili uwe na mvuto kwakila mtu.

Kusononeka sana


Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa blogu yako ya saikolojia wataalamu wa saikolojia wanatuhabarisha kuwa binadamu anapokuwa na hudhuni sana anaweza kuwa na hatari ya kupata magonjwa mbalimbali ikiwemo kisukari, moyo, kutokwenda haja kubwa, kupunguza nguvu za mapenzi, kupungua uzito wa mwili, kuumwa kichwa sana, kupoteza mwelekeo katika mipango yako ya kiakili nk.


Kwahiyo ndugu unatakiwa kujitahidi kufurahia maisha yako kila wakati na unapojaribu kuufanya mwili wako kufurahi, lakini hautaki watalaamu wanakushauri kuwa fanya mazoezi au jichanganye na watu mbalimbali katika maongezi hudhulia ibada za dini na mikutano mbalimbali ya injili hapo utaona mabadiliko ndugu yangu.


Wataalamu wanakuambia hivi usisononeke sana hata kama umeachwa na mpenzi wako, au wewe ni masikini, huna uwezo darasani, sauti yako unapoongea ni mbaya, unapofanya kazi uliyoisomea unakosea, au unapokumbana na mikasambalimbali ya maisha just toa hiyo huzuni moyoni mwako na kuanza kufurahia maisha hata kama ni mabaya ukifanya hivi utazoea na utaona kama kawaida. "Mungu akubariki sana"

Wednesday, November 5, 2008

Furaha ya Harusi


Binadamu ameumbwa na elementi chocgezi za kureta furaha, huzuni, hasira, kucheka, kuchukia n.k, lakini binadamu tuliowengi tukiwa tunafunga ndoa huwa tunajawa na fura kubwa sana, lakini baada ya kuanza kuishi na mke au mme furaha inapotea kunazuka kuchukiana na ugonviwakati mwingine.


Hii ni hatari kweli ndugu mpenzi msomaji wa blogu yako hii! ila kwa ushauri wangu nakuomba hata kama umeikia katika maisha ya kuishi na wako kipenzi nakuomba usimuchoke kwani kumuchoka ndiyo chanzocha ugonvi, kununiana, hasira nk.