Monday, December 15, 2008

Tabasamu ni nguvu ya penzi

IMEELEZWA kwamba mtu ambaye anatabasamu kila wakati huwa anaonekana mzuri na mtanashati kuzidi mtu ambaye saa zote yeye ni kununa tu. Wataalam mbalimbali wa masuala ya saikolojia wamefanya tafiti juu ya jambo hili na kubaini vitu kama hivyo.Wataalam kutoka Chuo Kikii cha Haverd nchini USA, walifanya utafiti na kubaini mtu ambaye ananuna kila wakati huwa anazeeka mapema na huonekana mbaya wa sura kutoka na sura yake kuzoea kujikunja.

Ikiwa naye Mtaalam wa Saikolojia ya Mapenzi Richard Athony wa Uingereza katika utafiti wake anasema "Wanawake wanaochukia ndoa zao wengi wanaoneka kama wazee kutokana na kutokuwa na raha Wanawake wanatakiwa kuzifurahia ndoa zao ili kuepuka kuzeeka mapema" alisema Mtafiti huyo na kuongeza kuwa: "Uzee huo unatokana na kukoswa raha kila wakati jambo ambalo linawasababisha kutokujijari ikiwemo kuoga vizuri na kujipodoa" Je wewe mfuatiliaji wa blogu yako ya saikolojia umefanya utafiti juu ya suala hili na umegundua kitu gani? Changia maoni yako.

1 comment:

MARKUS MPANGALA said...

kunoga tu mkuu leo nimepitia tu HABARI JA RERO WE MUJAMAAAAAA