Thursday, March 25, 2010

Utajitambuje Kama Unaakili???????????????????????


KWA mujibu wa Mwanasaikolojia mwenzangu Howard Gardiner aliandika kuwa binadamu wanatofautiana kiakili kila binadamu anauwezo wake katika kufikiri.

Sasa ndugu mpenzi wa blogu hii, utajitambuaje kuwa wewe unaakili kiasi gani? Wewe na wenzako munatofautiaje katika kufikiri? Kulingana na akili uliyonayo unatakiwa uwe nani na uishije katika dunia hii?

Jibu la maswali hapo juu ni kwamba ili kujitambua akili yako unatakiwa kuwafanya mahesabu ya akili yako. Na kwa mujibu wa Gardiner unatakiwa kufuata fomula hii hapa chini:

Chukua Akili ya Umri wako gawanya kwa Mtiririko wa Umri wako na Zidisha kwa Miamoja = Akili yako.

Akili= Mental Age (MA)            x    100
          Chronological Age (CA)

Kama mental age ni kubwa kuliko chronogical age jua kuwa akili yako iko juu zaidi ya kawaida, kama mental age iko sawa na chronological age jua kuwa akili yako ipo katika hali ya kawada na kama mental age iko chini ya chronological age jua kuwa akili yako iko chini ya kawaida.

Sasa jitambue wewe uko katika hali gani jifanyie uchunguzi ili kujitambua zaidi fanya mahesabu ya kujua akili yako ili uweze kujikonturo na maisha, jiwekee malengo kwa kufuatana na uwezo wako wa kufikiri. Ni hayo tu mpenzi wa blogu hii na kama unapenda zaidi kujifunza juu ya habari hii bonyeza katika kifungu cha kuchangia maoni na acha maelezo yako hakika nitayafanyia kazi.Zaidi kujitambua ni muhimu katika maisha yako

11 comments:

Simon Kitururu said...

Mental age mie huiona daima inutata na ndicho moja ya kinifanyacho nisiiamini hii fomwula ya akili.

Fita Lutonja said...

Saimon okay is good lakin kila kitu hapa dunia kinamapungufu hata ukiangalia kiti au kitu chochote utaona mapungufu yake.

Simon Kitururu said...

Kweli kabisaa ulichosema Mkuu FITA.

Fita Lutonja said...

Saimon okay is good lakin kila kitu hapa dunia kinamapungufu hata ukiangalia kiti au kitu chochote utaona mapungufu yake.

Fita Lutonja said...

poa saimon naona upo kwenye chakula chetu cha kila siku

Simon Kitururu said...

SI utani Mkuu FITA! Na kijiwechako ni moja ya CHAKULA kinisaidiacho kweli katika swala la mlo wa kila siku!:-(

Anonymous said...

"Chukua Akili ya Umri wako gawanya kwa Mtiririko wa Umri wako na Zidisha kwa Miamoja = Akili yako."

naomba utue maelezo ya kutosha kuhusu ya mahesabu cjakuelewa kabisaaa,fafanua zaidi nimependa hilo somo kwakweli.

hussein kaniki said...

nitajuaje sasa akili ya umri ? mkubwa sijakuelewa

Anonymous said...

Umenigusa halafu ukaniacha, napenda useme kuwa aunachukua umri, unapima na akili , sasa hapio ni kwenye nini? Mafanikio au kuwaza? Email yangu ni kisacha2003@yahoo.com

Unknown said...

hapo umeniacha njia panda mkuu mental age naipataje sasa nipe mfano

Godrick M Aluthe said...

toa mfano cjaelewa akili ntaipata wapi fafanua kwa undani na mfano pia kaka